HATIMAYE nguli wa sanaa za maigizo Bongo, Jacob Stephen Mbura ‘JB’ amelianika jimbo atakalogombea ubunge mwaka 2015.
JB aliyaongea hayo mwanzoni mwa wiki hii, jijini Dar es Salaam ambapo
alisema macho yake yote yapo Mkoa wa Dar es Salaam ambao una majimbo nane.
JB: Niliposema natangaza kugombea ubunge mwaka 2015 wengi waliamini
ni maneno tu, lakini nia yangu ni sahihi. Nitagombea na leo nasema
jimbo langu lipo Mkoa wa Dar es Salaam.
Aliongeza kuwa, jimbo atakalogombea litaendelea kubaki kuwa siri ya moyo
wake na meneja wake wa kampeni ambaye hakupenda kumtaja jina.
Majimbo yanaounda mkoa wa Dar es Salaam katika uwakilishi bungeni ni
Ukonga, Ilala, Kinondoni, Segerea, Kawe, Kigamboni, Ubungo na Temeke.
Kiukweli umefika wakati sasa wakurudisha fadila kwa mashabiki wangu
nahitaji kuwatumikia kwani na amini nikifanya hivyo hata kwa mungu
nitapata baraka alisema msanii huyo mwenye mashabiki wengi sana
Jb aliendelea kuieleza thesupestarstz kuwa kugombea kwake ubunge
kunaenda sambamba na hali halisi anayoiona kwa wananch watanzania na
kuongeza kuwa sasa tunatakiwa kuwa na hofu ya mungu kwa wananch wetu
wanaotuchagua kwa kura nyingi wakiamini wamepata mkombozi matokeo yake
wewe unawageuka ki ukweli inauma sana.
Thesuperstarstz imeongea na baadh ya wasanii wenzake kutaka kujua
wanalichukuliaje swala hilo ambapo wengi wameonyesha kumkubali jb na
kusema kama atafanikiwa kuwa mbunge basi utakuwa ni wakati mzuri sasa
kwa wasanii kupata mkombozi
|
No comments:
Post a Comment